Sentensi 5 kuhusu Mabomu mengine yaliyolipuliwa na Polisi Soweto Arusha leo June 18 2013
Maripota wetu kutoka Arusha wanaripoti
kwamba mabomu ya machozi yakipigwa na Polisi yameanza kusikika toka saa
kumi jioni kwenye eneo la Soweto.
Mmoja wa maripota hawa amesema wakati alipokua karibu na
mkusanyiko huo kuna Askari Polisi mmoja ambae alijichanganya na kuingia
katikati ya wafuasi wa Chadema ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu
wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa kwa mabomu na kufariki June 15
2013 na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa.
Baada ya hapo hawa Wafuasi hawakupenda kitendo cha Polisi
kujichanganya nao hivyo ikazuka kama kutoelewana huku wakitaka atoke,
baada ya dakika kadhaa huku pia Viongozi wa Chadema wakihutubia…. ndio
mabomu yakaanza kusikika.
Ripota wa pili anasema “Baada ya Tundu Lissu wa Chadema
kuhutubia na kusema chanzo cha vifo vya June 15 2013 ni Polisi, yani
vifo hivyo viliratibiwa na RPC Arusha… mabomu ya machozi ndio yakaanza
kulipuliwa”
0 comments:
Post a Comment