Pages

Tuesday, June 18, 2013

NMB wametisha!! wamezindua kitu kinaitwa Chap chap akaunti kwa ajili ya Watanzania wasio na akaunti

..
Mheshimiwa waziri wa fedha Dk William Mgimwa akichukuliwa alama za vidole na Ofisa mauzo ya Nje NMB Abdul Kandoro mara baada ya uzinduzi rasmi wa NMB chap chap akaunti mwishoni mwa wiki mkoani Dodoma

Benki ya NMB inaendelea kumiliki headlines kwa kubuni na kuboresha huduma za kibenki kuwawezesha wanafamilia kupata unafuu na urahisi wa upatikanaji wa huduma za kibenki Tanzania ambapo katika kulizingatia hili, mwishoni mwa wiki NMB si imezindua akaunti ya Chap Chap ambayo imelenga kuwafikia wanafamilia wote na kuwafungulia akaunti zao yani unafungua akaunti papo hapo na kupata kadi yake ya kutolea fedha ndani ya dakika  kumi.
.
Sehemu ya maofisa na wageni waalikwa kwenye uzinduzi huo.

      Mambo muhimu zaidi ambayo mteja wa Chap Chap anaweza kufaidika nayo ni pamoja na kuona salio la akaunti yako popote ulipo, kuweka fedha na kutoa fedha kwa mawakala wa M- pesa, kutuma fedha kwa wasio na akaunti mahali popote nchini kwa kutumia huduma ya Pesa Fasta, kununua vocha za muda wa maongezi kutoka kwenye mtandao wowote wa simu, kuchukua fedha hadi shillingi 1.000,000/= kutoka kwenye ATM
.
Ofisa mtendaji mkuu wa benki ya NMB Mark Wiessing akimshukuru waziri wa fedha Dk William Mgimwa mara baada ya kuzindua akaunti ya NMB Chap chap.

0 comments:

Post a Comment